Wednesday, January 9, 2013
On 4:37 AM by Shambani Solutions No comments
Sakata la uuzwaji wa ndege tatu za taasisi ya kilimo
anga jijini arusha lachukua sura mpya hasa baada ya waziri mwenye dhamana Mh
Chiza kuingilia kati na kuagiza kusimamisha uuzaji wa ngede iliyobaki.Pia Mh Chiza alienda mbali zaidi na kuagiza
uchunguzi ufanyike ili kubaini bei iliyotumika kuuza ndege hizo, zimeuzwa kwa
kampuni gani na ziko wapi kwa sasa ili hatua ziweze kuchukuliwa, pia Waziri Chiza alitoa maagizo hayo baada ya
kusikitishwa na hali ya taasisi ya kilimo anga pale alipotembelea tasisi hiyo
juzi na kukutana na mhandisi mkuu wa kituo hicho Gideon Mugusi.
Mbali na hilo pia mhandisi Mugusi alielezea na
matatizo mengine yanayokikabili kituo ikiwemo kukimbiwa na marubani wake 12 kwa
sababu ya kutafuta masilahi zaidi sehemu nyingine, kukosekana kwa fedha za
kendesha shughuli za kila siku.
Mwishoni katika kuonesha serikali ina mpango wa
kufufua kituo hicho Mh Chiza aliwaambia wadau kwamba serikali imetenga jumla ya
Tsh bil 1.5 ili kununua ndege zingine mpya ili zoezi la udhibiti wa wadudu
waharibifu liendelee kama ilvyokuwa zamani
Kwa taarifa
zaidi tembelea link hii:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment